Psalms 12

Kuomba Msaada

(Kwa Mwimbishaji: Mtindo Wa Sheminithi: Zaburi Ya Daudi)


1 a Bwana tusaidie, kwa kuwa wacha Mungu wametoweka;
waaminifu wametoweka miongoni mwa wanadamu.

2 bKila mmoja humwambia jirani yake uongo;
midomo yao ya hila huzungumza kwa udanganyifu.


3 c Bwana na akatilie mbali midomo yote ya hila
na kila ulimi uliojaa majivuno,

4 dule unaosema, “Kwa ndimi zetu tutashinda;
midomo ni mali yetu, bwana wetu ni nani?”


5 e“Kwa sababu ya uonevu wa wanyonge
na kulia kwa uchungu kwa wahitaji,
nitainuka sasa,” asema Bwana.
“Nitawalinda kutokana na wale
wenye nia mbaya juu yao.”

6 fManeno ya Bwana ni safi,
kama fedha iliyosafishwa katika tanuru,
iliyosafishwa mara saba.


7 gEe Bwana, utatuweka salama
na kutulinda na kizazi hiki milele.

8 hWatu waovu huenda wakiringa kila mahali
wakati ambapo yule aliye mbaya sana
ndiye anayeheshimiwa miongoni mwa watu.
Copyright information for SwhKC